🙏Je huwa unapambanaje na hali hii kuepuka hasara msimu huu,

👆Kwanza nishukuru kwa wote mliotoa michango yenu mbalimbali kuhusu swali langu hapo juu.

🙏Kwanza kabisa nini hutokea, Kipindi cha baridi, mwili wa mnyama mwenye damu moto, huhitaji Joto kusawaza kiwango cha joto la mwili

👈Hivyo hivyo kwa kuku,, huhitaji kiwango cha joto laziada kipindi hiki kukidhi joto la mwili (40°c)

👆👆 IKUMBUKWE
👉Kuku anaetaga anahitaji Enegy/ wanga kwaajili ya vitu viwili
🐣Production/Uzalishaji
🐣Maintanance/Kulinda mwili

👉Hivyo basi chakula anacho kula kuku, kinagawanyika sehemu hizo 2,

👆Wakati wa baridi kuku anahitaji kiwango kikubwa cha chakula kujilinda au kuzalisha joto la mwili, na kinachobaki ndicho hutumika kutengeneza yai

🐣Ikumbukwe kiwango cha chakula ulichokuwa unaliza wakati wa joto ndicho utakacho lisha wakati wa baridi, hivo lazima mayai yatapungua kutengenezwa kwa kua chakula kingine kinafanya kazi kubwa ya kulinda mwili

👉Utagaji hupungua sana msimu wa baridi kama hautakua unajua mbinu za kupunguza hali hii.


👉👈 KITAALAMU
👆Kuku wanapofika kuanza kutaga na kufikia asilimia 5% unaanza kuongeza chakula kwa kiwango cha uzalishaji( somo gumu kidogo litafata siku za mbele)

👉Sasa basi kupunguza adha hii unatakiwa kitaalamu , uongeze kiwango cha chakula kwenye gram ulizo kuwa unalisha kwa Siku( inashauriwa kuongeza gram 3-5) kwa wiki, hii itasaidia kuongeza kiwango cha Energy kwenda kuzalisha yai.

👉Pindi joto litakapo rejea unashauriwa kupunguza kiwango cha chakula Gram  1 kila siku katika zile za ziada ulizoongeza mpaka kufikia kiwango ulicho kuwa unalisha awali. Hii itasaidia kwa sehemu kupunguza adha ya kushuka kwa mayai au kusimama kabisa kutaga

👉Hili swala la uongezaji wa chakula utendaji kazi wake hutafautiana kulingana na umri wa kuku, na Inashauriwa chakula cha ziada kiongezwe asubuhi.

🙏NOTE

MBINU NYINGINE ZINAZO PENDEKEZWA, au Zilizo shauriwa na wafugaji wengine. (sijafanyia utafiti).

👉Waongezee kiwango cha mahindi mazima au Paraza yenye punje kubwa (mahindi huongeza kiwango cha Energy)

👉Mwanga masaa 16 yaani masaa 12 ya jua na uwashe taa sa 12 jioni na kuzima saa 4 usiku.


👉Weka cartens/ maturubai ya kuninginiza, kuzuia upepo wa baridi kuingia sana bandani (usizibe sana hewa iweze kuingia na kutoka )USIKU

👉Wengine wanasema wamekua wakiweka chanzo cha joto nyakati za usiku angalau kupunguza ubaridi bandani

👉Randa ziwe kavu, ili miguu na mwili vilale sehemu ambayo sio ya baridi sana au iliyo lowana

👉Wawekee egg booster formula Mara kwa Mara bila kusahau vitamins

👉👈👉👈👉👈👉👈