Ugonjwa huu huathiri kuku katika umri wowote na unapoingia kwenye kundi la kuku huweza kuua idadi kubwa ya kuku hao hadi kufikia 90%. Ndege wakubwa hustahimili kidogo kuliko wale wadogo kwasababu ya usugu mwilini (KINGA) uliojengeka kwa muda mrefu zaidi
Ugonjwa huu husababishwa na kimelea cha kirusi kiitwacho Avian paramyxovirus-1 na huenezwa kwa njia ya hewa na kugusana, kutokuwepo kwa usalama wa viumbe hai (biosecurity) katika shamba lako, uchafu unaoletwa na magari, viatu, vifaa vya kazi, ndege wa porini na watalii
DALILI ZAKE
Vifo vya ghafla muda mwingine bila hata kuonesha dalili
Kuvimba shingo na kichwa
Kupooza (paralysis) kwa mbawa na miguu
Ute hutoka mdomoni na puani
Kuku walioathirika hupata kizunguzungu
Kuharisha uharo wa kijani
Kuzubaa, kusinzia na mabawa kushuka
Kuzunguka kama vile ana kifafa
Utagaji hushuka na mayai kuwa na umbo lisilokuwa la kawaida
Zaidi ya 90% ya kuku huweza kufa
Kuku hufa kwa kupinda shingo
TIBA
Ugonjwa huu hauna dawa zaidi ya chanjo tu lakini unaweza kutumia TRIMAZINE 30% pamoja na Vitamini kwa kuku walioathirika
KINGA
Ugonjwa huu ukitokea jitahidi kuwatenga kuku wagonjwa na kuku wazima
Zuia muingiliano wa kutoka banda moja kwenda banda lingine pia weka maji yenye dawa (Farmguard) mlangoni kabla ya kuingia bandani na hakikisha unakanyaga hayo maji yenye dawa
Kideri kinauzuiwa kwa njia ya chanjo inayoitwa LASOTA.
Chanja kuku wako kila baada ya miezi mitatu na mara nne kwa mwaka. (Fuata mtiririko sahihi wa chanjo ya kideri)
Epuka kuingiza kuku wageni kutoka shamba usilolifahamamu na usilojua kuhusu historia ya chanjo
0 Comments