MAKALA JUU YA
CHANJO ZA KUKU WA AINA ZOTE.
Kuna aina tofauti za magonjwa kama MAGONJWA YA VIRUSI MAGONJWA YA BAKTERIA NA MAGONJWA YA KUPE/VIROBOTO/MINYOO.
MAGONJWA YA VIRUSI KWA KUKU NI KAMA
IBDauGUMBORO
MAREX
INFECTIOUS CORTYZA/MAFUA MAKALI
FOWL POX/NDUI
ILT ..INFECTIONS LARYNGOTRACHEITIS
NEWCASTLE/KIDELI
Magonjwa haya yasababishwayo na virusi HAYATIBIKI hivyo mfugaji ni vema ukawachanja kuku wako kwa moja ya mifumo ifuatayo....
CHANJO KIPINDI TU KUKU AKIWA
AMETOTOLEWA DAY OLD CHICK//HATCHERY ACHANJWE
Chanjo ya Mareks kwa kuku wa mayai...(l(SASSO ..KLOIRER...PURE LAYERS....BREEDER
ISIPOKUA PURE BROILERS))
Chanjo ya IBD/Gumboro
Chanjo NEWCASTLE/KIDELI
*MFUMO WA KWANZA*
SIKU YA KUMI CHANJO YA KIDELI/ND
SIKU YA 18 CHANJO YA GUMBORO/IBD
SIKU YA 28 CHANJO YA KIDELI/NEWCASTLE
SIKU YA 30 CHANJO YA NDUI/FOWL POX
KILA BAADA YA MIEZI MITATU AU WIKI 9 WAPE CHANJO YA KIDELI/NEWCASTLE HADI PALE UTAKAPO WATOA KUKU WAKO..
MFUMO WA PILI
SIKU YA SABA CHANJO YA KIDELI/NEWCASTLE
SIKU YA 14 CHANJO YA GUMBORO/IBD
SIKU YA 21 CHANJO YA NEWCASTLE//KIDELI
SIKU YA 30 CHANJO YA NDUI/FOWL POX
KILA BAADA YA MIEZI MITATI RUDIA CHANJO YA NEWCASTLE MPAKA UTAKAPO WATOA KUKU
NB+ Majina ya chanjo husika utajifunza kwa wauzaji wa madawa wanazijua hizo chanjo vizuri
VITU VYA KUZINGATIA WAKATI WA KUCHANJA KUKU
==Siku ya kuchanja kuku hakikisha kuku wametolewa maji asubuhi kabisa//uwanyime maji kwa Massaa 3au4
==Vyombo vyako vya kuwekea chanjo vioshwe vizuri kwa maji safi.
==Maji ya kuwekea chanjo yawe masafi na yachanganywe na Coper au chlorex blue ili kuondoa chlorine ya kwenye maji kufanya chanjo iwe na nguvu.
==Chanjo iliyotunzwa kwenye friji ichanganywe kwenye maji kutokana na uwingi wa kuku::Mara nyingi kopo moja la chanjo ni kwa kuku 500 dozi ndogo na 1000 dozi kubwa kwahio angalia unakuku wangapi alafu wachanganyie maji watakayo weza kumaliza.
==Wape maji yenye chanjo kwa muda wa saa1 hadi masaa2 alafu toa maji yenye chanjo.
==Dakika 5 baada ya kuweka chanjo angalia kama kuku wote//vifaranga wote wamekunywa maji yenye chanjo kwa kutazama midomo yao itakua na rangi ya yale maji yenye copper.
==Kama kuna kifaranga hajanywa maji yachanjo mnyweshe kwa kijiko,,,au syrynge(bomba la sindano).
Chanjo ya ndui huchomwa kwa sindano kwenye bawa nivema umuite mtaalamu akuelekeze
BROILERS HAWACHANJWI FOWL POX/Ndui
HII NDIO MAKALA JUU YA RATIBA SAHIHI YA CHANJO
IMEANDALIWA NA GREYSON KAHISEMTAALAMU WA UFUGAJI WA KUKU 0769799728 kwa maelezo na mawasiliano zaidi.


0 Comments